LANGUAGE :
English | Swahili

Karibu sana!

Sikika ni shirika lisilo la kiserikali lililosajiliwa nchini Tanzania mwaka 2000. maono ya sikika ni huduma bora za afya kwa kila mtanzania.

 

Sikika huwawezesha wananchi kushirikiana vema na watoa huduma za afya kwa kupitia uhamasishaji wa ushiriki wa jamii, uwazi, na uwajibikaji katika mifumo ya utoaji huduma za afya katika ngazi ya wilaya. Sikika pia hufanya kazi pamoja na bunge na wizara kuu zinazo husika kuboresha mipango ya taifa ya afaya pamoja na bajeti. Kwa sasa sikika hupatika Dar es salaam na Kibaha miji yote hii ikiwa katika ukanda wa pwani ya Tanzania

Majibu ya maswali kama

Serikali ina mpango gani wa kudhibiti maabukizi ya vvu / ukimwi, bajeti ya secta ya afya ikoje, wananchi wana mtazamo gani juu ya huduma za afya nchini Tanzania na je wanachi wanajua haki zao?  Yanapatikana katika tovuti yetu pamoja na machapisho. halikadhalika jarida letu litakuwa linakupa taarifa juu ya kazi zetu, maendeleo pamoja na changamoto.

MAENEO YA PROGRAMU

  • Usimamizi wa Afya na Fedha
  • Rasilimali Watu Katika Afya
  • Madawa na Ugawaji
  • VVU na UKIMWI

Usimamizi wa Afya na Fedha

  • Uwazi katika bajeti
  • Ufanisi wa bajeti
  • Usimamizi

Rasilimali Watu Katika Afya

  • Maadili
  • Kupelekwa na kuhifadhi
  • Mfumo wa malalamiko

Madawa na Usanbazaji

  • Usambazaji
  • Upatikanaji
  • Usambazaji

VVU na UKIMWI

  • Uwazi
  • Upatikanaji na usambazaji
  • Mipango
  • Baada ya uchaguzi mkuu wa kugombea urais uliofanyika tarehe 31 Oktoba 2010, Serikali ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia taasisi, idara na mashirika mbalimbali ya umma ilitumia shilingi 175,639,750 kwa ajili ya kutoa salamu 217 za pongezi zilizochapishwa katika vyombo mbalimbali vya habari kama magazeti kuanzia tarehe 8 Novemba hadi 8 Decemba 2010. Fedha hizo singeweza kununua vitanda 828 au utoaji wa vifaa 1254.

  • Asilimia 48 ya wilaya zilizofanyiwa utafiti hazikuwa na bandeji za ‘absorbent gauze’. Asilimia 8 tu ya wilaya hizo zilikuwa na kiasi cha kutosha cha bandeji hizo. Vile vile asilimia 37 ya hivyo havikuwa na bandeji hizo kabisa. Asilimia 10 kwa muda wa miezi mitatu hadi mitano. Hali hii ilikuwa hivyo kwa kipindi cha miezi mitatu hadi sita kabla ya utafiti. (Chanzo: Ripoti ya Upatikanaji wa Dawa na Vifaa vya Tiba ya Mwaka 2011)

  • Ripoti inaonyesha makada wa nane kati ya 15 wameonyesha kiwango chini cha mahudhuriao kwa asilimia 80. Kati 328 ya wahitimu wa vyuo vikuu ambao walipangwa maeneo ya mijini kama sehemu zao za kufanyia kazi, waliripoti watu 305 ambao ni sawa na asilimia 93. Lakini kwa wilaya zilizopo vijijini, asilimia 26 ya wahitimu wa vyuo vikuu hawakuripoti katika sehemu zao walizopangiwa kufanya kazi. (Chanzo: Rasilimali kwa ajili ya kupeleka somo la Afya -2010)

Machapisho Mapya

Machapisho zaidi