


Karibu sana!
Sikika ni shirika lisilo la kiserika lililosajiliwa nchini Tanzania kwa lengo la kufanya ushawishi na utetezi juu ya utawala bora katika sekta ya afya. Shirika lilianzishwa mwaka 1999 likijulikana kama Youth Action Volunteers (YAV), na baadaye lilikua na kubadilika kutoka katika utetezi wa afya ya uzazi kwa vijana na kujikita kwenye maeneo makuu ya msingi katika sekta ya afya ambayo ni: Utawala na Usimamizi wa Fedha za Afya, Rasilimali Watu katika Afya, Madawa na Vifaa tiba pamoja na UKIMWI na Virusi vya UKIMWI. Kwa sasa, tumeimarisha shughuli zetu katika maeneo ya vijijini ambayo ni Kondoa na Mpwapwa (Dodoma), Kiteto na Simanjiro (Manyara), Iramba na SingidaVijijini (Singida) ili kukukuza na kuimarisha juhudi zilizokuwa zinatekelezwa awali mijini na kwenye miji midogo ikijumuisha wilaya za Dar es Salaam na Kibaha. Tumeendelea kufanya utafiti mbalimbali wa kisayansi na kutumia matokeo na shuhuda za tafiti hizo kufanya utetezi katika ngazi zote za utoaji wa huduma za afya.Vilevile tunatambua wananchi wote kama watumia huduma za afya. Hivyo basi, tunawezesha wanajamii wenyewe kushiriki kikamilifu katika Kusimamia Uwajibikaji na Kutathmini utoaji wa huduma za afya katika ngazi zote (SAM). Sikika inatumia mfumo mpya wa kupima matokeo (Outcome Mapping) katika kufuatilia na kutathmini matokeo ya kazi mbalimbali za shirika kwenye sekta ya afya. Mafanikio ya shughuli zetu za utetezi yanatokana na ubora wa tafiti tunazofanya pamoja na ushirikiano wa karibu na wadau mbalimbali zikiwemo asasi za kiraia. |
MAENEO YA PROGRAMU
Usimamizi wa Afya na Fedha
Rasilimali Watu Katika Afya
Madawa na Usanbazaji
VVU na UKIMWI
|