


Tunafanya nini |
Tunafanya NiniKupitia shuguli mbalimbali zilizopangwa kuanzia January mwaka 2011 hadi desemba mwak 2015, sikika hutafuta kuwezesha wananchi kuelewa na kushiriki katika kufanya maamuzi katika masuala yanayohusu afya zao katika ngazi ya wilaya na taifa. Kufanya hivi sikika hufany kazi pamoja na watoa huduma, mamlaka za wilaya na watunga sera katika wilaya nne katika jiji la Dar es salaam (kinondoni, ilala, temeke na Kibaha). Shuguli zitafanyika katika kata 35, kata 10 katika wilaya tatu za dar es salaam na kata 5 katiak wilya ya Kibaha. Shuguli hizi zipo chini ya idara tatu ambazo ni “usimamizi wa huduma za afya na fedha”, “madawa na usambazaji”, “rasilimali watu kwa afya”, habari na machapisho”, na usimamizi na tathimini ya vvu/ ukimwi. Tafadhali rejea hapo chini kupata sampuli ya shuguli za sasa za sikika. Kwa taarifa zaidi rejea mapango kazi wa sikika wa mwaka 2011. Vipindi vya redioTunaendesha vipindi vya redio kila wiki ili kuhamasisha ushiriki wa vijana katika masuala ya uwajibikaji katika secta ya vvu na ukimwi. Jarida la sikikaTunaanda jarida mara nne kwa mwaka, kwa kupitia jarida hili tunaweza kuwasiliana na kusambaza taarifa ya vitu tulivyojifunza kutokana na tafiti zake vikiwemo vipindi vya mafunzo pamoja na taarifa zozote zinazohusu usimamizi wa afya na sera za afya. Kushiriki kuandaa wilaya nne za cchp kwa mwaka 2009/10Tunawezesha vijana kushiriki “kamati za mtaani” katika kata zao ili wajadili na kukusanya taarifa zinazohusiana na vipaumbele vya huduma za afya katika kata zao, kamati hizi ni za kudumu na zinaundwa na jamii husika kujadili na kusimamia masuala yote ambayo yanahusu jamiii husika. Usimamizi wa CCPHSikika husimamia utekelezaji wa ccph ilikuhakikisha bajeti iliopangwa na mipango yote intekelezwa kama ilivyopangwa kwa manufaa ya jamii husika Kushirikiana na madiwanina mamlaka za wilayaMadhumuni ya mpango huu ni kukuza ushiriki wa madiwani pamoja na mamalaka za wilaya ili waweze kuwasimamia watendaji wao kwa mfano: kuhakikisha upangaji yakinifu wa bajeti ya secta ya afya, kufanya tathmini katika uwajibikaji katika wilaya nne pamoja na kuhamasisha usaswa katika huduma za afya katika maeneo husika ikiwemo kupanga na mgawanyo wa rasilimali, kusimamia matumizi, usimamizi wa utendaji kazi, pamoja na usimaizi wa upatikanaji kwa njia rahisi wa huduma za afya, lengo likiwa ni kupata rasilimali zote za huduma za afya za mwaka ujao, kutathmini ufanisi wake katika ugawaji na kama ugawaji unaendana na sera na mipango iliowekwa na kama mbinu za awali zimeongeza ufanisi katika kupanga bajeti na ugawaji wa rasilimali. Kushirikiana na wabungeLengo ni kuongeza uwezo wa bunge kufanya serikali iwajibike kwa kushirikiana na tathmini yetu ili kuboresha mipango na sera ya secta ya afya hususa vvu na ukimwi. Ili kuleta ufanisi tunawasidia kufuatilia utendaji wa mipango na mapendekezo ambayo yaliwekwa katika secta ya afya na utekelezaji wa secta ya afya kwa kamati husika. Vyombo vya habariKukakisha kuwa tathini zetu juu ya secta ya afya pamoja na utawala na sera zinawafikia wanajamii wengi na hibua mijadala. Tunafanya vipindi mabali mbali ili kutoa taarifa za changamoto pamoja na fursa ambazo tunakutana nazo katika kufuatilia, maeneo yanayo husika ni pamoja na: utendaji wa serikali, ufuatiliaji na ukaguzi wa mahesabu, na bunge. Maeneo mengine ni pamoja na utendaji wa secta ya afya katika upangaji, utendaji, na bajeti. |