LANGUAGE :
English | Swahili

Karibu sana!

 

Sikika ni shirika lisilo la kiserika lililosajiliwa nchini Tanzania kwa lengo la kufanya ushawishi na utetezi juu ya utawala bora katika sekta ya afya. Shirika lilianzishwa mwaka 1999 likijulikana kama Youth Action Volunteers (YAV), na baadaye lilikua na kubadilika kutoka katika utetezi wa  afya ya uzazi kwa vijana na kujikita kwenye maeneo makuu ya msingi katika  sekta ya afya ambayo ni: Utawala na Usimamizi wa Fedha za Afya, Rasilimali Watu katika Afya, Madawa na Vifaa tiba pamoja na UKIMWI na Virusi vya UKIMWI.

Kwa sasa, tumeimarisha shughuli zetu katika maeneo ya vijijini ambayo ni Kondoa na Mpwapwa (Dodoma), Kiteto na Simanjiro (Manyara), Iramba na SingidaVijijini (Singida) ili kukukuza na kuimarisha  juhudi zilizokuwa zinatekelezwa awali mijini na kwenye miji midogo ikijumuisha  wilaya za Dar es Salaam na Kibaha.

Tumeendelea kufanya utafiti mbalimbali wa kisayansi na kutumia matokeo na shuhuda za tafiti hizo kufanya utetezi katika ngazi zote za utoaji wa huduma za afya.Vilevile tunatambua wananchi wote kama watumia huduma za afya. Hivyo basi, tunawezesha wanajamii wenyewe kushiriki  kikamilifu  katika Kusimamia Uwajibikaji na Kutathmini utoaji wa huduma za afya katika ngazi zote (SAM).

Sikika inatumia mfumo mpya wa kupima matokeo (Outcome Mapping) katika kufuatilia na kutathmini matokeo ya kazi mbalimbali za shirika kwenye sekta ya afya. Mafanikio ya shughuli zetu za utetezi yanatokana na ubora wa tafiti tunazofanya pamoja na ushirikiano wa karibu na wadau mbalimbali zikiwemo asasi za kiraia. 

MAENEO YA PROGRAMU

  • Usimamizi wa Afya na Fedha
  • Rasilimali Watu Katika Afya
  • Madawa na Ugawaji
  • VVU na UKIMWI

Usimamizi wa Afya na Fedha

  • Uwazi katika bajeti
  • Ufanisi wa bajeti
  • Usimamizi

Rasilimali Watu Katika Afya

  • Maadili
  • Kupelekwa na kuhifadhi
  • Mfumo wa malalamiko

Madawa na Usanbazaji

  • Usambazaji
  • Upatikanaji
  • Usambazaji

VVU na UKIMWI

  • Uwazi
  • Upatikanaji na usambazaji
  • Mipango
  • Baada ya uchaguzi mkuu wa kugombea urais uliofanyika tarehe 31 Oktoba 2010, Serikali ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia taasisi, idara na mashirika mbalimbali ya umma ilitumia shilingi 175,639,750 kwa ajili ya kutoa salamu 217 za pongezi zilizochapishwa katika vyombo mbalimbali vya habari kama magazeti kuanzia tarehe 8 Novemba hadi 8 Decemba 2010. Fedha hizo singeweza kununua vitanda 828 au utoaji wa vifaa 1254.

  • Asilimia 48 ya wilaya zilizofanyiwa utafiti hazikuwa na bandeji za ‘absorbent gauze’. Asilimia 8 tu ya wilaya hizo zilikuwa na kiasi cha kutosha cha bandeji hizo. Vile vile asilimia 37 ya hivyo havikuwa na bandeji hizo kabisa. Asilimia 10 kwa muda wa miezi mitatu hadi mitano. Hali hii ilikuwa hivyo kwa kipindi cha miezi mitatu hadi sita kabla ya utafiti. (Chanzo: Ripoti ya Upatikanaji wa Dawa na Vifaa vya Tiba ya Mwaka 2011)

  • Ripoti inaonyesha makada wa nane kati ya 15 wameonyesha kiwango chini cha mahudhuriao kwa asilimia 80. Kati 328 ya wahitimu wa vyuo vikuu ambao walipangwa maeneo ya mijini kama sehemu zao za kufanyia kazi, waliripoti watu 305 ambao ni sawa na asilimia 93. Lakini kwa wilaya zilizopo vijijini, asilimia 26 ya wahitimu wa vyuo vikuu hawakuripoti katika sehemu zao walizopangiwa kufanya kazi. (Chanzo: Rasilimali kwa ajili ya kupeleka somo la Afya -2010)

Machapisho Mapya

Machapisho zaidi